Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Bakar Hamad Bakar (12 total)

MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu haya mazuri, lakini pamoja na mjibu haya na jitihada hizi za Serikali kupitia juhudi hizi za Serikali ambazo zinafanyika kupitia Mabalozi wetu mbalimbali naomba kufahamu, ni bidhaa zipi hasa za kilimo ambazo zimetangazwa kupitia Mabalozi wetu na zimepata soko kubwa zaidi nje ya nchi yetu? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bakar Hamad Bakar, Mbunge wa Baraza la Wawakilishi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, list hii ni kubwa sana, lakini itoshe tu kusema kwamba kwa mazao yanayoongoza ni parachichi, soya na mazao mengine kama vile matunda na mbogamboga, ahsante sana.
MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana pia nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wa sekta hii ya uvuvi kwenye Pato la Taifa kwa kiwango cha asilimia 1.8, tunakubaliana kwamba mchango huu bado ni mdogo sana, lakini nafahamu kwamba ipo mipango ya Serikali kununua meli kwa ajili ya uvuvi wa Bahari Kuu. Nataka kufahamu ni stage gani tumefikia kwenye uagizaji wa meli hizi kwenda kuvua kwenye Bahari Kuu?

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nataka kujua ni kwa namna gani mipango hii ya Serikali kwenye Wizara hii ya Uvuvi inaishirikisha Zanzibar katika kukuza Uchumi wa Bluu? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Bakar Hamad Bakar. Swali lake la kwanza anataka kujua kuhusu mchango.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba mchango huu ni mdogo, mchango wa asilimia 1.9 ni mchango mdogo na ndiyo maana Serikali imekuja na mikakati mbalimbali ambayo itakuja kusaidia sana kuinua kipato hiki. Moja ya mikakati ambayo Serikali imekuja nayo ni pamoja na ujenzi wa Bandari ya Uvuvi. Tunakwenda kujenga Bandari ya Uvuvi pia kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya kuchakata mazao ya samaki, pia kufufua viwanda ambavyo tayari vimeshakufa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba asilimia 1.9 ni asilimia ndogo na Serikali iko na mkakati wa kufanya kazi hiyo ikiwa ni pamoja na kufufua Shirika la TAFICO ambalo tayari limeshakufa. Kwa hiyo, tunayo mikakati kama Serikali kwamba mikakati hiyo ambayo tumeiweka tukiitimiza vizuri tunaweza tukaongeza pato kutoka 1.9 kwenda juu zaidi. Kwa hiyo nimwombe Mheshimiwa Mbunge avute subira kwamba iko mikakati Serikali inajipanga kwa ajili ya kwenda kuimarisha jambo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ametaka kujua ni lini ununuzi wa meli hiyo utakamilika. Mchakato wa ununuzi wa meli upo unaendelea lakini umesimama kidogo kwa sababu za kibajeti. Kwa hiyo, mara Serikali itakapopata fedha ununuzi wa meli hiyo utaweza kufanyika mara moja. Ahsante.
MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii nami niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ninataka kujua ni mpango upi wa Serikali kuweka miundombinu shindani kwenye Chuo hiki cha Hali ya Hewa Kigoma; hasa ukizingatia kwamba chuo hiki kwa nchi za Afrika ni nchi chache sana ambazo zinatoa taaluma hii na sisi kuweza kulitumia hilo soko la kuweza kupokea wanafunzi kutoka nchi mbalimbali Afrika? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bakar Hamad kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali tumejipanga vyema kukiboresha chuo hiki ili kiwe shindani katika nchi za Afrika Mashariki na Kati na ukizingatia kwamba hiki ni chuo pekee kinachotoa elimu hii ya hali ya hewa; na kwa msingi huo tumeingia makubaliano na Chuo cha Usafirishaji nchini (NIT) ili kianze kutoa elimu ya TEHAMA lakini zaidi ya yote kwa sababu pia Chuo chetu cha NIT kitaanza kutoa mafunzo ya urubani na mafunzo ya urubani yanaendana na hali ya hewa. Kwa hiyo, hata hiki pia kitakuwa sehemu ya hayo mafunzo; na zaidi ya yote pia chuo chetu tunakitangaza hata nchi jirani kwa maana ya Rwanda pamoja na Burundi, ahsante.
MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Nyumba za Askari katika kambi ya Askari Mfikiwa ni chakavu sana. Je, ni upi mpango wa Serikali katika kuziboresha nyumba zile?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye jibu la msingi tunatambua uwepo wa uchakavu wa vituo na makazi ya Askari. Kama nilivyokwishakusema ni mpango wa wizara kufanya ukarabati wa majengo hayo kutegemeana na uwepo wa bajeti. Mwaka huu tutaanza na yale ambayo yapo kwenye kipaumbele tutaendelea na ukarabati kadri miaka inavyokwenda kulingana na upatikanaji wa fedha nashukuru.
MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa hii ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa ni ahadi ya CCM ya kuimarisha ushirikiano baina ya Wizara hizi ambazo siyo za Muungano. Je, Wizara ya Afya inashirikianaje na Wizara ya Afya ya Zanzibar kwenye kutatua changamoto hizi za Watoto Njiti? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, anachokisema Mbunge ni kweli na nimejaribu kutembelea baadhi ya maeneo upande wa Taifa letu upande wa Visiwani ni kweli kunahitajika maboresho makubwa sana kwenye huduma za afya. Jana Mheshimiwa Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alikuwa anajadiliana na baadhi ya wadau ili kuona ni namna gani hawa wadau ambao wanatoa huduma huku upande wa Bara waweze kwenda upande wa pili wa visiwani na kuweza kuboresha miundombinu ya afya badala ya kupeleka fedha kwenye maeneo hayo. Tayari AMREF wamekubali kuelekea upande huo wa pili kwa ajili ya kuboresha maeneo unayosema Mheshimiwa Mbunge.
MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana mimi nilitaja kujua tu kwamba je, Wizara hii ya Muungano na Mazingira ni kwa kiasi gani inashirikiana na Wizara ya Makamu wa Kwanza wa Rais ambayo pia nayo inashughulikia masuala ya mazingira katika kukabiliana na suala hili la changamoto ya gesi ukaa au hewa ukaa?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kama tunavyofahamu kwamba Ofisi ya Makamu wa Rais ina deal na masuala ya Muungano Bara na Visiwani, Lakini masuala ya mazingira upande wa Zanzibar ni chini ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais. Hata hivyo tunafahamu kwamba ajenda ya mazingira ni ajenda mtambuka haina mipaka, ndiyo maana muda wote tumeweza kushirikiana vya kutosha kabisa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais na ndiyo maana hata ukiangalia miradi mingine tunayoiandika katika bajeti yetu Madam Maryam pale Mbunge wa Pandani anafahamu kwamba katika jambo tulijadili katika kikao chetu katika Kamati yetu ya Bunge, miongoni mwa mambo jinsi gani miradi mbalimbali inaenda mpaka kule Zanzibar na hata hivyo ndiyo maana leo hii tuna miradi Kaskazini A, na hata mradi wa Sepwese pale tunaenda kujenga ukuta pale hii yote ni suala zima la mpango wa pamoja jinsi gani tunashughulika na ajenda ya mazingira katika maeneo yetu.
MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii nami niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ninataka kujua ni mpango upi wa Serikali kuweka miundombinu shindani kwenye Chuo hiki cha Hali ya Hewa Kigoma; hasa ukizingatia kwamba chuo hiki kwa nchi za Afrika ni nchi chache sana ambazo zinatoa taaluma hii na sisi kuweza kulitumia hilo soko la kuweza kupokea wanafunzi kutoka nchi mbalimbali Afrika? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bakar Hamad kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali tumejipanga vyema kukiboresha chuo hiki ili kiwe shindani katika nchi za Afrika Mashariki na Kati na ukizingatia kwamba hiki ni chuo pekee kinachotoa elimu hii ya hali ya hewa; na kwa msingi huo tumeingia makubaliano na Chuo cha Usafirishaji nchini (NIT) ili kianze kutoa elimu ya TEHAMA lakini zaidi ya yote kwa sababu pia Chuo chetu cha NIT kitaanza kutoa mafunzo ya urubani na mafunzo ya urubani yanaendana na hali ya hewa. Kwa hiyo, hata hiki pia kitakuwa sehemu ya hayo mafunzo; na zaidi ya yote pia chuo chetu tunakitangaza hata nchi jirani kwa maana ya Rwanda pamoja na Burundi, ahsante.
MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri kwamba je, fedha zilizotengwa za ujenzi wa upanuzi wa uwanja wa ndege Pemba zimejumuisha pia malipo ya fidia kwa wananchi ambao wameingia kwenye eneo hilo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Bakar Hamad kuhusu uwanja wa Pemba; katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha utakaoanza mwezi wa Julai na tunashukuru Bunge lilipitisha tumetenga fedha kwa ajili ya upanuzi wa uwanja kwa Pemba lakini pamoja na fidia eneo lile ambalo tutatwaa kwa ajili ya ujenzi huo.
MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa hii ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa ni ahadi ya CCM ya kuimarisha ushirikiano baina ya Wizara hizi ambazo siyo za Muungano. Je, Wizara ya Afya inashirikianaje na Wizara ya Afya ya Zanzibar kwenye kutatua changamoto hizi za Watoto Njiti? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, anachokisema Mbunge ni kweli na nimejaribu kutembelea baadhi ya maeneo upande wa Taifa letu upande wa Visiwani ni kweli kunahitajika maboresho makubwa sana kwenye huduma za afya. Jana Mheshimiwa Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alikuwa anajadiliana na baadhi ya wadau ili kuona ni namna gani hawa wadau ambao wanatoa huduma huku upande wa Bara waweze kwenda upande wa pili wa visiwani na kuweza kuboresha miundombinu ya afya badala ya kupeleka fedha kwenye maeneo hayo. Tayari AMREF wamekubali kuelekea upande huo wa pili kwa ajili ya kuboresha maeneo unayosema Mheshimiwa Mbunge.

MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, na pia napongeza kwa majibu haya ya Serikali. Naomba kupata ufafanuzi kwa maswali mawili. Moja, nilitaka kujua kwa sababu uchumi wa watu wa kwenye ukanda huu wa bahari hususan Pemba, Unguja, Tanga, Mtwara na Lindi wanategemea sana upatikanaji wa usafiri wa baharini. Ni lini fedha hizi zitapatikana ili kwenda kufanikisha upatikanaji wa Meli hiyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, mbili; kwa kuwa Ilani ya CCM inahimiza zaidi kwenye ushirikiano baina ya taasisi ambazo siyo za Muungano, ni maeneo yapi ya ushirikiano ambayo Kampuni hii ya Meli ya Tanzania inashirikiana na Shirika la Meli la Zanzibar? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bakar, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, moja, kuhusu ni lini mchakato utakamilika wa upembuzi yakinifu, tumeshaingiza kwenye bajeti katika mwaka huu wa fedha 2023/2024. Tunategemea kabla hatujakamilisha mwaka huu, tutakuwa tumeshakamilisha upembuzi yakinifu kwa kujua lini, kiasi gani, na kwa namna gani pengine inapaswa ifanyike?

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, ameuliza swali kuhusu ushirikiano kati ya Kampuni ya Meli ya Tanzania (ATCL) pamoja na ile ya SHIPCO (Shirika la Meli la Zanzibar). Tumeshaanza katika hatua za awali ushirikiano kati ya pande hizi mbili na yapo maeneo makuu matatu ambayo tunaweza kuyatazama katika hatua za kuanzia. Moja, tunaangalia ushirikiano katika taarifa na wataalam; pili, tunaangalia uwezo na kuwajengea uwezo wataalam wetu katika sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na mabaharia, TEHAMA, mipango, utafiti, rasilimali watu pamoja na masoko; tatu, tutaongeza zaidi kwenye eneo la kubadilishana uzoefu katika pande zote mbili.
MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, elimu ya juu ni sekta ya Muungano na kwa kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Mwinyi ameitangaza Pemba kwamba ni eneo maalum la uwekezaji. Je, ni upi mpango wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano kupitia Wizara hii wa kuwekeza kwenye sekta hii ya elimu kwa kujenga Chuo Kikuu Pemba? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Bakar Bakar, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli anachozungumza Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara hii ni Wizara ya Muungano hasa hasa kwenye masuala ya elimu ya juu, lakini kama nilivyokwishaeleza katika maswali yaliyopita, katika mradi wetu wa HEET tunakwenda kufanya ujenzi mkubwa katika eneo lile la Zanzibar kwa upande wa Chuo chetu kile cha Marine Institute ambapo nacho vilevile kitatengeneza branch baadaye katika Kisiwa cha Pemba.

Mheshimiwa Spika, naomba nimwondoe wasiwasi kwa kadri muda utakavyokwenda, tutaifikia Pemba. Hivi sasa mkakati uliopo vilevile chuo chetu cha masafa marefu, hiki Chuo Kikuu Huria tayari kina branch pale Pemba na katika mgao huu kimenufaika na maeneo ambayo yanakwenda kuboreshwa ni pamoja na tawi letu lile la Chuo Kikuu Huria pale katika Kisiwa cha Pemba ambacho nacho vilevile ni chuo kikuu kwa mujibu wa sheria.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.
MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mchakato wa mabadiliko ya sheria hii ili kuweza kufanya vyombo vya usafiri kutambulika hapa Tanzania Bara umeonekana umechukua muda mrefu sana, sasa ni kwa nini Serikali haioni haja ya kuweka mwongozo maalumu kipindi hiki wakati tunasubiria mabadiliko ya sheria hiyo?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bakar, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, kwa kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zipo katika mazungumzo, naomba tuwe na subira na utaratibu uliopo kwa sasa uendelee kutumika. Pale mazungumzo yatakapokamilika, basi marekebisho yatafanyika ili kuhakikisha kwamba vyombo vinasajiliwa kwa pamoja.