Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Questions to the Prime Minister from Hon. Selemani Moshi Kakoso (1 total)

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Awali ya yote nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi kubwa ambayo anaifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kuuliza swali kwako Mikoa ya Kanda ya Magharibi, Mkoa wa Rukwa, Katavi, Tabora na Kigoma, ni Mikoa pekee ambayo hayaijaunganishwa barabara kwa kiwango cha lami. Mikoa hii inazalisha chakula kwa wingi, kwa bahati mbaya bado miundombinu kuwasaidia wananchi wa Mikoa hii ambayo walisahaulika kwa kipindi kirefu toka uhuru? (Makofi)
Naomba kupata majibu ya Serikali juu ya umuhimu wa kuimarisha miundombinu ya kujenga barabara kwa kiwango cha lami na ukizingatia Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, amewaahidi wananchi hao na mkoa wake wa kwanza wakati wa harakati za kuomba kura za Urais alianzia Mkoa wa Katavi na kutoa ahadi nzito, Serikali ina dhamira ipi ya kukamilisha miundombinu hiyo? (Makofi)iko duni na kuwafanya wananchi wa mikoa hii kudumaa kiuchumi.
Je, Serikali ina mpango gani ya kuunganisha hii mikoa ili iweze kupata barabara za lami, kwa maana ya barabara kutoka Sumbawanga kuja Mpanda, barabara kutoka Mpanda kwenda Kigoma, barabara kutoka Mpanda kupitia Wilaya ya Mlele-Sikonge kwenda Tabora, halikadhalika kumalizia barabara ya Tabora kwenda Kigoma. Serikali ina mpango gani
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Selemani Kakoso, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Mkoa ule hatujamudu kuunganisha maeneo yote na mikoa yote ya jirani. Hata hivyo, Mheshimiwa Mbunge anajua jitihada ambazo Serikali hii inafanya sasa za kuimarisha miundombinu na hasa barabara kwa miradi tuliyonayo nchi nzima, yenye malengo ya kuunganisha mikoa yetu tuliyonayo. Tayari ipo miradi inaendelea Mkoani Katavi ya kuunganisha na mikoa ya jirani, ikiwemo Katavi kwenda Mbeya. Pia upo mpango wa ujenzi wa barabara kutoka Katavi kupitia Sikonge mpaka Tabora na tunaimarisha barabara kutoka Katavi kwenda Kigoma kupitia Uvinza na maeneo mengine.
Mheshimiwa Spika, miradi hii ambayo sasa inatekelezwa nchi nzima, inawezekana yako maeneo ambayo tumeanza na mengine tunaendelea, lakini mengine yapo kwenye mpango wa uendelezaji. Kwa hiyo, nataka nimpe imani na hii niwaambie wananchi wote walioko mikoa ile kwamba Serikali inayo nia ya dhati ya kuhakikisha kwamba tunaunganisha mikoa yetu yote kwa barabara za kiwango cha lami. Kazi tunayoifanya sasa ni kuhakikisha tu kwamba, tunatenga fedha kwa barabara ambazo zinaendelea, lakini zile ambazo hatujaanza kabisa, tunapeleka wataalam kwa ajili ya upembuzi yakinifu ili tuanze michoro na kazi hiyo tuweze kuanza. (Makofi)
Kwa hiyo, tutaendelea pia kushirikiana na wananchi wa Mkoa wa Katavi kuhakikisha kwamba barabara zao zote tunaziunganisha, kama ambavyo sasa tunaendelea kuunganisha mikoa mingine kama Mkoa wa Dodoma na Manyara, Dodoma na Iringa, Dodoma tumeshaanza kwenda Singida sasa tunakwenda Tabora kupitia Manyoni. Kwa hiyo jitihada hizi ni za nchi nzima na wote ni mashahidi kwamba kazi hizi zinaendelea vizuri.
Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kazi hiyo inaendelea na Katavi pia watanufaika pia na mpango wa Kitaifa wa kuunganisha mikoa yetu.