Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 56 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 2 2017-06-29

Name

Flatei Gregory Massay

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya uhakiki wa watumishi ambao wana vyeti fake. Sasa baada ya uhakiki huo wengine wameacha vituo vya afya na zahanati zetu kule.

Sasa swali langu, je, lini mtaajiri sasa, ili watu wetu kule wapate huduma, hasa kwenye maeneo ya afya ambako watumishi wameshaacha kazi kutokana na kwamba, walikuwa wana vyeti ambavyo havistahili kuendelea kuwepo? Ahsante.

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Mbulu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tumepitisha zoezi hili la uhakiki wa vyeti kwa watumishi wetu na uhakiki huu baada ya kuwa tumekamilisha tulipata makundi matatu. Kundi la kwanza ni wale wenye vyeti fake moja kwa moja, kundi la pili ni wale wenye vyeti vinavyotumika na zaidi ya mtu mmoja, lakini kundi la tatu uko utata wa majina ambao umejitokeza kwenye vyeti hivi ambavyo wao wamepata nafasi ya kukata rufaa. Sasa wote hawa wameacha pengo kwa sasa, na ndilo ambalo Mheshimiwa Mbunge amelizungumzia, lini tunatoa ajira.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli ametoa nafasi za ajira zaidi ya 50,000 ili kuziba mapengo haya ambayo yamejitokeza kwa wenye vyeti fake, lakini vilevile ili kuongeza tu ajira kwenye sekta nyingine kwa lengo la kuboresha utoaji huduma kwenye sekta mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, tayari vibali vimeshatolewa na Wizara ya Utumishi, tumeanza na idara ya elimu, tumesha ajiri walimu wa masomo ya sayansi wamekwenda kwenye vituo, tumetoa pia nafasi kwenye sekta ya afya na vibali hivi vitaendelea kutolewa kadri ya nafasi ambazo Mheshimiwa Rais ameahidi kwa Watanzania.

Mheshimiwa Spika, ninaamini Rais wetu mpendwa kwa ahadi yake nafasi hizi ataendelea kuzitoa ili tuzibe mapengo na kuboresha pale ambako kuna upungufu mkubwa. Na sasa ajira hizi zitaenda kitaaluma zaidi, ili kuweza kuleta ufanisi mkubwa kwenye sekta y ajira. Ahsante.

Additional Question(s) to Prime Minister