Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 8 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 2 2020-02-06

Name

Mary Pius Chatanda

Gender

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Mheshimiwa Waziri Mkuu TARURA imekuwa ikifanya kazi kubwa ya kutekeleza miradi ya barabara mijini na vijijini. Na kwa kuwa umuhimu wa barabara hizi ndizo zinazochangia kwa kiasi kikubwa uchumi katika usafirishaji. Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa bahati mbaya sana TARURA wanakumbwa na bajeti ndogo. Je, Serikali itakuwa tayari sasa kuiongezea bajeti TARURA ili iweze kutekeleza majukumu yake haya makubwa ambayo imekabidhiwa? (Makofi)

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Chatanda Mbunge wa Korogwe Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tunacho chombo kinachosimamia ujenzi na ukarabati wa barabara vijijini; TARURA kwa sasa; ambacho tumekipa mamlaka ya kufanya kazi karibu kwa pamoja na Mamlaka ya Serikali za Mtaa kwa maana ya halmashauri za wilaya. Sasa kila TARURA iliyoko kwenye halmashauri hiyo jukumu lake ni kufanya mapitio ya barabara zote zilizopo ndani ya wWilaya hiyo kuona mahitaji ya ujenzi wake, ukarabati wake na matengenezo ya kila siku pale ambako panahitaji ukarabati huo na kutenga fedha na kuomba fedha kulingana na mahitaji yake. Kwa hiyo kila TARURA katika kila halmashauri inayo bajeti yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, inawezekana pia TARURA Wilaya ya Korogwe haitoshelezi mahitaji ya ukarabati wa barabara zake. Si rahisi kupata bajeti yote kwa asilimia 100 kulingana na mahitaji hayo lakini bado kipindi tulichonacho sasa mwezi wa pili tukiwa tunaelekea kwenye Bunge la Bajeti kuanzia mwezi wa nne basi TARURA ile kwenye halmashauri husika ioneshe mahitaji ya fedha kulingana na mahitaji ya barabara zao ili sasa tuanze kuingiza kwenye mpango wa fedha kwa ajili ya matumizi ya mwaka ujao wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo niseme Serikali iko tayari kupokea maombi ya TARURA zote nchini za mahitaji ya fedha halafu tutazigawa sote kwa pamoja; na kupitia Kamati yetu ya Miundombinu inaweza kusimamia pia TARURA kupata fedha ya kutosha ili iweze kujenga barabara zake kwenye maeneo yake kama ambavyo halmashauri inahitaji kuboresha barabara zake. Ahsante. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister