Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 34 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 5 2019-05-23

Name

Richard Phillip Mbogo

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa usikivu wake ilisikia kilio ambacho Wabunge pamoja na wananchi kuhusiana na migogoro ya ardhi ambayo imehusisha vijiji zaidi ya 360 katika muingiliano wa mipaka kati ya vijiji pamoja hifadhi za taifa au hifadhi za misitu au hifadhi za misitu au mapori tengefu n kupelekea hivyo Mheshimiwa Rais aliunda kamati ya Mawaziri nane wakiongozwa na Mheshimiwa Lukuvi katika kuratibu na kumshauri namna bora ya kutatua changamoto hii ya vijiji hivi zaidi ya 360, vikiwemo Vijiji vya Mataweni na Stalike katika Jimbo la Nsimbo.

Mheshimiwa Spika, ningependa kujua, je, Serikali ipo tayari kukaa kwa pamoja na Wabunge kupitia taarifa hiyo ikiwa ni namna ya kufanya reconciliation ili kusiwe na malalamiko tena ya baadaye kwa sababu hili ni zoezi ambalo litakuwa linatatua kwa muda mrefu. Je, Serikali ipo tayari kukaa na Wabunge kupitia kabla ya kumkabidhi Mheshimiwa Rais ripoti hiyo?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbogo, Mbunge wa Nsimbo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge anataka kujua kama ripoti ya ukaguzi wa ardhi ya Tume iliyoundwa na Mheshimiwa Rais kama inaweza kuja kushirikisha Wabunge hapa.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tumekuwa tukipata taarifa mbalimbali za migogoro ya ardhi kwenye maeneo kadhaa. Wizara ya Ardhi imefanya kazi nzuri ya kupita maeneo yote yenye migogoro ya ardhi na mwisho Mheshimiwa Rais aliunda timu ya Mawaziri wanane kupita maeneo yote yenye migogoro kukagua na kusikiliza maoni ya wananchi kwenye maeneo hayo ili kuweza kuratibu vizuri na hatimaye tuweze kutoa utatuzi wa migogoro hiyo. Sasa timu ile ni ya Mheshimiwa Rais, matokeo ya ukaguzi wake yatawasilishwa kwa Mheshimiwa Rais kwanza kabla ya kupelekwa mahali pengine, kiitifaki inatakiwa iwe hivyo.

Mheshimiwa Spika, lakini pia timu ile ilipokuwa inapita kwenye maeneo yale, tuliwaagiza Mawaziri watoe taarifa kwenye Mamlaka za Wilaya kule ili watu/wadau wote washirikishwe kule, tuna amini kama kulikuwa na Wabunge na wakati ule ulikuwa siyo wakati wa Bunge, mliweza kushiriki kwa namna moja au nyingine. Pia Mheshimiwa Rais ikimpendeza, baada ya kupata taarifa hiyo, anaweza kutujulisha lakini sasa kiitifaki kwanza aliyetaka tume iundwe ndiye ambaye ambaye tunaweza kumpelekea kwanza, hatuwezi kuileta Bungeni kwanza bila kumpelekea Mheshimiwa Rais mwenyewe kiitifaki. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hilo litaangaliwa na kama Mheshimiwa Rais itampendeza anaweza akaamua kutushirikisha lakini tuna amini Wabunge kwa taarifa tulizopeleka kule kwenye halmashauri zenu ili muweze kushiriki katika kutambua na kusaidia kueleza migogoro na kama ambavyo mmekuwa mkieleza hapa ndani, yale maoni yenu ya hapa ndani ndiyo yaliyochukuliwa na kwenda kuyafanyia kazi, ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister