Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 49 Other Sectors Maswali kwa Waziri Mkuu 14 2016-06-23

Name

Richard Phillip Mbogo

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, ina sera nzuri, ina sheria mbalimbali juu ya elimu ambazo zinapelekea wanafunzi wa Kidato cha Nne waliofaulu, wanachaguliwa na kwenda Kidato cha Tano. Mara nyingi kwa maarufu wamesema huwa kunakuwa na selection.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kuna habari ambazo zinazagaa kwamba mwaka huu Serikali haitachukua wanafunzi kutokana na sababu ambazo bado hazijaeleweka. Sasa je, Mheshimiwa Waziri Mkuu, jambo hili lina ukweli gani? Kama lipo, Serikali inatoa kauli gani juu ya suala hilo?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

imiwa Mbogo, Mbunge wa Nsimbo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nataka nikanushe kwamba Serikali haina mpango wa kuwapanga vijana wetu waliomaliza Kidato cha Nne kwenda Kidato cha Tano. Najua tuna makundi mengi ya watu wanapenda kupotosha tu habari, ikiwemo na hii, lakini nataka nitumie nafasi hii kuwahakikishia wanafunzi wote waliomaliza Kidato cha Nne, wanaopaswa kwenda Kidato cha Tano, lakini na wazazi pia wa vijana wetu hawa kwamba Wizara ya TAMISEMI yenye dhamana na Sekondari, kwa pamoja na Wizara ya Elimu, kazi ya upangaji wa vijana wanaokwenda Kidato cha Tano inaendelea na wakati wowote ule mwishoni mwa mwezi huu majina hayo yatakuwa yametoka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi zinazofanywa sasa, nyie wote mnatambua kwamba mwaka uliopita wanafunzi hawa walikuwa wanapangwa kwa mfumo wa GPA na sasa tumebadilisha GPA kwenda division. Kwa hiyo, kazi ambayo Wizara ilikuwa inafanya ni kubadilisha ule mfumo wa GPA kwenda division ili uweze kuwapanga vizuri kwa division zao na sifa ambazo zinatakiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la upangaji halikuwa ni kwa ajili ya Kidato cha Tano peke yake, kuna wale ambao tunawapeleka Vyuo kama Afya, Kilimo na maeneo mengine, nao pia wanatakiwa wapangwe kwa mfumo wa division na wote hao unapowapanga Kidato cha Tano, ili wengine waweze kupangwa, zoezi hili lazima lifanywe kwa pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kazi hii inakamilika, itatoka muda mfupi ujao na kwa hiyo, baada ya hapo Serikali itatoa majibu haya wiki mbili kabla ili kuwawezesha wazazi kujipanga vizuri kuwapeleka vijana wao kwenye maeneo mengine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kulikuwa na kazi ya sensa ya kuhakikisha tuna shule ngapi za Kidato cha Tano ili tuweze kuwapeleka vijana wetu wote. Kwa sababu mwaka huu ufaulu ni mkubwa zaidi, kuliko mwaka jana, 2015. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, lazima tuhakikishe tunawapeleka vijana kulingana na uwezo wa shule ili tujue tumewapeleka wangapi na wanaobaki wangapi wenye stahili ya kwenda Kidato cha Tano ili nao wapate nafasi ya kupangiwa maeneo mengine kwa stahili ile ile ya Kidato cha Tano ili waziweze kupoteza ile stahili yao waliyokuwanayo ya Kidato cha Tano; kama vile kuwapeleka kwenye course za miaka mitatu za Diploma ambapo miaka miwili huitumia kwa ngazi ya Kidato cha Tano na cha Sita, wakishafaulu wanaingia kwa profession, kama ni afya, kama ni kilimo, kama ni sekta nyingine; kwa mfano Ualimu, ili waweze kuendelea na stahili yao ya Kidato cha Sita. Kwa hiyo, kazi hiyo itakapokamilika, tutaweza kutoa taarifa mapema.

Additional Question(s) to Prime Minister