Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 sitting 3 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 2 2016-01-28

Name

Selemani Moshi Kakoso

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Awali ya yote nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi kubwa ambayo anaifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kuuliza swali kwako Mikoa ya Kanda ya Magharibi, Mkoa wa Rukwa, Katavi, Tabora na Kigoma, ni Mikoa pekee ambayo hayaijaunganishwa barabara kwa kiwango cha lami. Mikoa hii inazalisha chakula kwa wingi, kwa bahati mbaya bado miundombinu kuwasaidia wananchi wa Mikoa hii ambayo walisahaulika kwa kipindi kirefu toka uhuru? (Makofi)
Naomba kupata majibu ya Serikali juu ya umuhimu wa kuimarisha miundombinu ya kujenga barabara kwa kiwango cha lami na ukizingatia Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, amewaahidi wananchi hao na mkoa wake wa kwanza wakati wa harakati za kuomba kura za Urais alianzia Mkoa wa Katavi na kutoa ahadi nzito, Serikali ina dhamira ipi ya kukamilisha miundombinu hiyo? (Makofi)iko duni na kuwafanya wananchi wa mikoa hii kudumaa kiuchumi.
Je, Serikali ina mpango gani ya kuunganisha hii mikoa ili iweze kupata barabara za lami, kwa maana ya barabara kutoka Sumbawanga kuja Mpanda, barabara kutoka Mpanda kwenda Kigoma, barabara kutoka Mpanda kupitia Wilaya ya Mlele-Sikonge kwenda Tabora, halikadhalika kumalizia barabara ya Tabora kwenda Kigoma. Serikali ina mpango gani

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Selemani Kakoso, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Mkoa ule hatujamudu kuunganisha maeneo yote na mikoa yote ya jirani. Hata hivyo, Mheshimiwa Mbunge anajua jitihada ambazo Serikali hii inafanya sasa za kuimarisha miundombinu na hasa barabara kwa miradi tuliyonayo nchi nzima, yenye malengo ya kuunganisha mikoa yetu tuliyonayo. Tayari ipo miradi inaendelea Mkoani Katavi ya kuunganisha na mikoa ya jirani, ikiwemo Katavi kwenda Mbeya. Pia upo mpango wa ujenzi wa barabara kutoka Katavi kupitia Sikonge mpaka Tabora na tunaimarisha barabara kutoka Katavi kwenda Kigoma kupitia Uvinza na maeneo mengine.
Mheshimiwa Spika, miradi hii ambayo sasa inatekelezwa nchi nzima, inawezekana yako maeneo ambayo tumeanza na mengine tunaendelea, lakini mengine yapo kwenye mpango wa uendelezaji. Kwa hiyo, nataka nimpe imani na hii niwaambie wananchi wote walioko mikoa ile kwamba Serikali inayo nia ya dhati ya kuhakikisha kwamba tunaunganisha mikoa yetu yote kwa barabara za kiwango cha lami. Kazi tunayoifanya sasa ni kuhakikisha tu kwamba, tunatenga fedha kwa barabara ambazo zinaendelea, lakini zile ambazo hatujaanza kabisa, tunapeleka wataalam kwa ajili ya upembuzi yakinifu ili tuanze michoro na kazi hiyo tuweze kuanza. (Makofi)
Kwa hiyo, tutaendelea pia kushirikiana na wananchi wa Mkoa wa Katavi kuhakikisha kwamba barabara zao zote tunaziunganisha, kama ambavyo sasa tunaendelea kuunganisha mikoa mingine kama Mkoa wa Dodoma na Manyara, Dodoma na Iringa, Dodoma tumeshaanza kwenda Singida sasa tunakwenda Tabora kupitia Manyoni. Kwa hiyo jitihada hizi ni za nchi nzima na wote ni mashahidi kwamba kazi hizi zinaendelea vizuri.
Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kazi hiyo inaendelea na Katavi pia watanufaika pia na mpango wa Kitaifa wa kuunganisha mikoa yetu.

Additional Question(s) to Prime Minister

Name

Selemani Moshi Kakoso

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nishukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, swali langu la nyongeza; kwa kuwa mvua zinazoendelea kunyesha katika mikoa hiyo ni nyingi na zimeharibu miundombinu. Serikali ina mpango upi wa dharura kuhakikisha mikoa hii inapata huduma ili katika kipindi inapojipanga waweze kupeleka huduma itakayosaidia kutatua matatizo ya barabara ambazo zimeharibika sana?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kakoso, Mbunge wa Mpanda Vijijini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Kakoso, ni shahidi kwamba juzi tulipata taarifa kutoka Katavi, kwamba barabara zetu kule zimekatika kutokana na mvua nyingi. Hakuna mawasiliano sasa ya kutoka Mpanda, kwenda Tabora kupitia Sikonge, hakuna mawasiliano kutoka Mpanda kwenda Kigoma kupitia Uvinza, hata tuta la reli nalo limetetereka.
Mheshimiwa Spika, tulichofanya juzi tumechukua hatua za haraka na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano amefanya kazi hiyo vizuri, amepeleka Wataalam, hapa ninapozungumza wataalam wapo pale wanaimarisha barabara ile, ili kuweza kurudisha mawasiliano. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini kwa kuwa mvua zinaendelea tumeamua tutafute njia nzuri, ambayo itakuwa na uhakika wa kuunganisha mawasiliano kati ya Mpanda na mikoa ile pamoja na Tabora kwa kurudisha reli, njia ya treni kutoka Dodoma itakwenda Tabora - Kaliua ili iweze kwenda Mpanda. Ile sehemu ya tuta ambalo lilikuwa limeharibika tumeshakamilisha na tayari tumeliambia Shirika la Reli, wauze tiketi Dar es Salaam, abiria wote wanaokwenda Mpanda wapewe mabasi waletwe Dodoma kupanda treni inayokwenda Mpanda.
Mheshimiwa Spika, hiyo ndio njia ambayo tumeamua tuitumie sasa ili kuimarisha usafiri wa kwenda Mpanda; huku Tanroad wakiendelea na ukarabati wa barabara zote ambazo zimekatika na malengo yetu barabara hizo tuziimarishe ili ziweze kupitika wakati wote.