Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 21 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 3 2022-05-12

Name

Joseph Anania Tadayo

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Mheshimiwa Waziri Mkuu hivi karibuni Serikali yetu imeonesha uwezo mkubwa sana wa kushughulika na masuala na miradi mikubwa katika hali ya dharura na kwa mafanikio makubwa sana. Mfano mojawapo ikiwa ni miradi mbalimbali iliyoendeshwa kwa hizi fedha za UVIKO na hata linaloendelea sasa hivi la kudhibiti madhara ya bei za mafuta kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini Mheshimiwa Waziri Mkuu lipo tatizo la muda mrefu la uchakavu wa Shule za Msingi ambazo nyingine zilijengwa wakati wa ukoloni nchi nzima. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu ni kwamba je, Serikali haioni kwamba kwa uwezo huu ulionao kwamba sasa ichukulie suala la uchakavu wa hizi shule za msingi kwamba ni jambo la dharura ili shule hizi zikarabatiwe na elimu yetu iendelee kuwa bora.

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tadayo Mbunge wa Mwanga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tuna shule za muda mrefu sana na wala siyo shule za msingi tu, ziko shule za sekondari, vyuo vya elimu ya kati hata vyuo vikuu. Nakiri kwamba tunahitaji mkakati wa Serikali wa dharura lakini utaratibu wa kukarabati shule hizi kongwe tayari ulishaanza kwa kupeleka fedha kwenye shule zetu ili kukarabati miundombinu yake irudi katika hali inayoweza kutumika kisasa zaidi. Tulianza zoezi hilo mwaka 2013 kwa kupeleka milioni 50, kila shule ili kukarabati na kuongeza fedha, tukaongeza uwezo zaidi wa Serikalini, tumeendelea kutoa fedha kwa ajili ya ukarabati shule za msingi kongwe, sekondari kongwe, FDC kongwe lakini pia hata VETA ambazo zilianza kujengwa muda mrefu na vyuo vikuu vyote vilivyo vikongwe nchini.

Mheshimiwa Spika, zoezi hili ni endelevu ndani ya Serikali ya Serikali. Kwa hiyo, udharura ni pale ambapo labda kutatokea madhara makubwa moja kati ya miundombinu hiyo tunaweza tukapeleka fedha, lakini kila mwaka tunatenga fedha. Hata Wizara ya Elimu jana wameshatoa bajeti zao moja kati ya fedha ambayo jana tumeitisha hapa ni ya kukarabati shule zote kongwe na taasisi zote za elimu ili miundombinu hii iweze kutumika vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Waheshimiwa Wabunge wote ambao pia kwenye majimbo yenu kuna hizo shule hizo kongwe na Watanzania naona pia kuna vijana wetu wa shule, shule zotte na taasisi zote zitakarabatiwa. Waheshimiwa Wabunge mmeshapitisha bajeti zetu hapa na naomba muendelee kupitisha bajeti za Wizara zote ili Serikali ifanye kazi yake ikiwemo na ukarabati wa shule hizo. Ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister