Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 26 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 3 2022-05-19

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Waziri Mkuu kumekuwa na malalamiko makubwa sana hapa nchini kwa ndugu zetu, Watanzania wenzetu waliokuwa watumishi Serikalini walioondolewa kwa kigezo cha kutokuwa na cheti cha form four.

Sasa ni lini watalipwa stahiki zao halali za kiutumishi ambazo wanadai ili waweze kupeleka watoto wao shule na wengine waweze kujitibisha? Nini kauli ya Serikali? (Makofi)

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cherehani, Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo ulipata taarifa wiki moja iliyopita agizo ambalo lilitolewa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan juu ya msamaha alioutoa kwa wale wote waliokuwa wameondolewa kwenye utumishi, waliokuwa wametambulika kama wameghushi vyeti vya kidato cha nne na wametumikia katika nchi hii kwamba sasa tufanye mapitio tuwatambue. Pia alitoa fursa la kuunda timu kutoka Wizara ya Utumishi na Utawala Bora kwa pamoja na TAMISEMI ili kuwatambua wale wote waliotumikia kwenye nchi hii na kutoa agizo kwamba walipwe asilimia tano ya pension walikuwa na mchango kwenye pension waliokuwa wanaichangia ili waweze kulipwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Tume ile itakapokamilisha kazi tutayatambua haya yote, idadi yao, halafu pia wangapi, wale wote ambao wanastahili kupata hiyo asilimia tano ya mchango waliokuwa wanauchangia, lakini pia kuona makundi mengine na maelekezo yanayotolewa.

Mheshimiwa Spika, sasa kwa kuwa Mheshimiwa Rais ameunda Tume naomba nisitoe majibu juu ya hilo tuiache Tume ifanye kazi yake, halafu tutapata majibu sahihi. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister