Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 26 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 5 2022-05-19

Name

Francis Leonard Mtega

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwakuwa baadhi ya maeneo yenye migogoro na hifadhi za Taifa hayajajumuishwa kwenye ile Kamati ya Wizara nane na hata mengine yaliyojumuishwa nayo uamuzi bado haujatolewa na Serikali.

Je, ni lini sasa zoezi hili litaanza rasmi na kumalizika ili wananchi waendelee na shughuli zao bila wasiwasi? Ahsante. (Makofi)

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mtega, Mbunge wa Mbarali kama ifuatavyo:- (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru umenipa nafasi ya kulijibu swali hili kwa sababu timu ya Mawaziri wanane kutoka Wizara zile shiriki imeendelea kufanya kazi ya kutambua maeneo yote yenye mgogoro na kazi hii tulianza mwaka 2019. Tayari tumeshaainisha maeneo yote na tulileta taarifa hapa Bungeni ya vijiji vilivyofikiwa vilivyokuwa na migogoro lakini katika kutatua migogoro hii iliyopo kati ya wakulima na wafugaji, wakulima na wananchi na hifadhi, lakini pia hata maeneo ya ulinzi tumeweza kuratibu vizuri na ile timu pia hata wiki iliyopita ilikuwa imesafiri kwenda kukamilisha hiyo kazi na kazi bado inaendelea.

Mheshimiwa Spika, migogoro hii ina ngazi mbalimbali na sisi Serikali tumeweka utaratibu; kwanza migogoro yote ya ardhi inaratibiwa na ngazi za vijiji kwanza kwenye maeneo yenye migogoro, na zile kamati zinao uwezo wa kumaliza migogoro hii kwa kukutanisha wenye migogoro, lakini pia ngazi ya Kata, ngazi wa Wilaya na Mkoa. Leo tunazungumzia Wizara nane matatizo yanayoshughulikiwa na Wizara hizi nane ni yale makubwa tu, ambayo yanahitaji pia kukutanisha wataalam wa ngazi za Wizara na ndio kwa sababu Wizara nane zote zinazunguka na kupitia migogoro ile mikubwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nilitaka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunaendelea na kazi ya kuondoa migogoro inayojitokeza kwenye maeneo yetu na tunafanikiwa kwa kiasi kikubwa na tunaendelea kubainisha maeneo yenye migogoro yenye tija na yasiyokuwa na tija, lengo hapa ni kuwataka Watanzania kila mmoja afanye kazi yake, wale wakulima waendelee kufanya kazi zao, wanaoshughulikia mifugo, uvuvi na maeneo mengine, lakini pia hata hifadhi zetu nazo zifanye kazi yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na kwenye hifadhi wote mnatambua Serikali hii pia ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, imeridhia maeneo yale ya hifadhi ambayo kwa sasa yanaonekana hayana tija tunayaruhusu wananchi wafanye shughuli zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo utaratibu huu unaendele kuratibiwa na pindi watakapokamilisha tutakuja kutoa taarifa kwenye Bunge lako tukufu ili Waheshimiwa Wabunge mnaotoka kwenye maeneo hayo muwe na taarifa hiyo. Kwa hiyo tutakamilisha wakati wowote tu kwa haraka zaidi ili na nyie mpate taarifa na migogoro iishe kwenye maeneo yetu. Ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister