Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 31 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 4 2022-05-26

Name

Kenneth Ernest Nollo

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Spika, nchi nyingi duniani zimerusha satellite angani kwa matumizi mbalimbali ikiwemo kupata takwimu sahihi za hali ya hewa. Katika anga la Afrika kwa sasa tuna satellite 41 na kati ya hizo 41 mbili zinatoka katika mataifa ya Afrika Mashariki. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuanza na programu ya kutengeneza satellite na baadaye tuweze kuirusha katika anga letu?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kenneth Nollo, Mbunge wa Bahi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa anahitaji kujua maendeleo ya teknolojia kwenye mawasiliano. Ameeleza kwamba nchi nyingine tayari zimejitegemea katika kununu mitambo inayowezesha nchi husika kuboresha mawasiliano yake. Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zinaendelea kwa kasi katika maboresho ya TEHAMA, na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kazi moja kubwa aliyoifanya ni kuanzisha Wizara ya Sayansi, Mawasiliano na Teknolojia ambayo pia ina habari mawasiliano na teknolojia ya habari ambayo pia inaendelea kufanya ufuatiliji wa maeneo ambayo tayari tunayo na maeneo ambayo bado hayapo kwa lengo la kufanya maboresho. Na Wizara, kama ambavyo inaendelea kufanya kazi yake na imeshapitishiwa bajeti yake, na Waziri hapa ameeleza maboresho makubwa yaliyofanywa nchini. Lengo hii teknolojia kufikisha kwa Watanzania mpaka vijijini. Tumeanza na teknolojia ambayo inawezesha kufanya mawasiliano maeneo yote, na tunapanua wigo huu mpaka kwenye ngazi za kimataifa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka nikuhakikishie kwamba maeneo yote ambayo nchini sasa hayapo ambayo yanahitajika katika kuboreshwa mfumo mzima wa mawasiliano Serikali itafanya maboresho kutafuta fedha zaidi kwa ajili ya kuhakikisha kwamba teknolojia tunaipandisha na teknolojia inawafikia wananchi wote mpaka kule vijiji, ahsante. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister