Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 3 Education, Science,Technology and Vocational Training, Maswali kwa Waziri Mkuu 2 2023-11-02

Name

Husna Juma Sekiboko

Gender

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana.

Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwanza nikupongeze sana kwa Serikali kukamilisha mchakato huu na leo kutuletea rasmi kwamba nchi yetu inakwenda kutekeleza Sera na Mtaala Mpya, lakini Mheshimiwa Waziri Mkuu katika maelezo yako umeeleza kwamba Mtaala huu unakwenda kujikita katika Elimu ya Ujuzi. Hata hivyo, tuna upungufu mkubwa wa vifaa vya kufundishia katika level zote primary, secondary na Elimu ya kati kwa maana ya vyuo vya kati.

Je, Serikali inajipanga vipi kwenda kuhakikisha kwamba tunapata Makarakana na vifaa vya kufundishia vya kutosha ili kuweza kutekeleza mtaala huu?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Husna, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tumeeleza kwamba elimu sasa isiwe ya kitaaluma pekee bali iingize masuala ya ujuzi kwa lengo la wanaomaliza elimu ya msingi hii ambayo imeenda mpaka kwenye sekondari ngazi ya chini, wanapomaliza wawe wana ujuzi ambao wanaweza wakaanza pia kuingia kwenye ujasiriamali moja kwa moja. Sasa Serikali imejipangje kupata vifaa vya kufundishia, tumeeleza kwenye Sera na kwa kuwa Sera itatekelezeka mwaka 2027, bado Serikali itaendelea kutafuta uwezo wa kuanza kununua vifaa na kupeleka kwenye maeneo haya.

Mheshimiwa Spika, sisi sasa tumeanza ujenzi wa VETA, Vyuo vya Ufundi, lakini pia tuna Vyuo vya Wananchi (FDCs) ambavyo pia vyenyewe vinatoa elimu ya ujuzi. Kwa hiyo kwa kipindi hiki cha mpito tunaanza kuimarisha Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi, Vyuo vyetu vya VETA ambavyo wanajenga kila Wilaya kwa lengo la kuanza kutoa ujuzi huku tukijipanga kutafuta vifaa na kupeleka kwenye shule zetu za sekondari. Kama Sera inavyosema mafunzo ya mali na ufundi tutaanza na kidato cha kwanza. Kwa hiyo tuta-concentrate, tutaongeza nguvu katika kutoa vifaa na hasa katika kuongeza bajeti na tutaleta maombi yetu hapa kwenu Waheshimiwa Wabunge, naomba mridhie bajeti zetu ili tuweze kununua vifaa tupeleke sekondari na tutafanya hivyo awamu kwa awamu ili tufikie malengo ambayo tunayakusudia. Hii ndio namna ambayo tunakusudia kuitekeleza ili tuweze kufikia mafanikio, ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister