Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 8 Industries and Trade Maswali kwa Waziri Mkuu 1 2024-02-08

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Gender

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na jitihada kubwa ambayo Serikali inafanya ya kuhakikisha kwamba Nchi yetu inakuwa na sukari ya kutosha wakati wote, lakini katika siku za hivi karibuni kumekuwa na taharuki na upungufu wa sukari kiasi cha wananchi kuwa na malalamiko. Vilevile, ikizingatiwa kwamba katika kipindi hiki cha karibuni tunategemea kuwa na mfungo wa Ramadhan na Kwaresma, kwa hiyo wananchi wanakuwa na hofu juu ya suala hilo.

Je, ni lini kauli ya Serikali ili wananchi waweze kuondokana na hofu hiyo? (Makofi)

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Stella Manyanya, Mbunge wa Mbamba Bay, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tuna upungufu wa sukari nchini na upungufu huu umetokana na kuwepo kwa mvua nyingi ambazo maeneo yetu ya mashamba ya miwa inayozalisha sukari maji yamejaa kiasi cha kwamba, wale wa miliki wa mashamba haya hawawezi kutoa miwa kutoka mashambani kupeleka viwandani na kule viwanda vimebaki havina sukari.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa upungufu huu umeishafanyiwa kazi na Wizara ya Kilimo na Waheshimiwa Wabunge na Watanzania mmepata kumsikia Mheshimiwa Waziri wa Kilimo akitoa maelezo hapa ya nini Serikali inafanya ili kukabiliana na upungufu huu ili Watanzania na wananchi kwa ujumla waweze kutumia bidhaa hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja Wizara imetoa vibali kwa Wafanyabiashara mbalimbali wakiwemo wazalishaji wa sukari wenyewe. Kuingiza sukari nchini zaidi ya tani laki moja na zoezi hilo linaendelea na taarifa ambazo ninazo kutoka Wizara ya Kilimo tayari tumeanza kupata sukari kutoka nje. Hii itaendelea kupunguza makali ya kukosekana kwa sukari nchini ili Watanzania waweze kutumia bidhaa hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia tumeendelea kukaa na viwanda kuona namna bora ya kupata bidhaa hii pale ambako mvua zinapungua ili waendelee kuzalisha, upungufu huu siyo wa muda mrefu na kipindi hiki tunaamini tutafika mpaka kipindi cha Ramadhan. Kwa hiyo ndugu zetu Waislam watafunga Ramadhan na Serikali itawahakikishia kwamba sukari itakuwepo nchini, ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister