Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 42 Community Development, Gender and Children Maswali kwa Waziri Mkuu 3 2024-06-06

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL E. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi hii ya kuuliza swali kwa Waziri kwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Waziri Mkuu, hapa nchini Serikali imekuwa ikitoa 10% ya mikopo kwa walemavu, wanawake, lakini pia vijana ambao wako chini ya miaka 35, lakini kuna kundi hili ambalo linazidi miaka 35 ambalo ndio mhimili mkubwa wa familia na ndio walipa ada wakubwa kwa watoto na ndio wanaotibisha familia, lakini pia ndio kundi ambalo linalinda uchumi wa familia.

Sasa ni nini mkakati mkubwa wa Serikali wa kuweza kulikumbuka kundi hili katika masuala ya mikopo? Ahsante.

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cherehani, Mbunge wa Ushetu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali imetenga fungu maalum la mapato ya ndani katika kila halmashauri kutoa fursa za kuendeleza ujasiriamali kwa kutoa mikopo midogo midogo na ya kati kwa makundi ya wanawake 4%, walemavu 2% na vijana 4%. Sasa kundi hili la zaidi ya miaka 35 sio kwamba tumelisahau bali tunazo fursa nyingine za kupata mitaji kupitia mifuko mbalimbali, lakini pia kwenda kwenye taasisi za fedha kama vile mabenki na ile mifuko ambayo imepata vibali maalumu vya kukopesha.

Mheshimiwa Spika, haya makundi tunayoyazungumza kutokana na tathmini za ndani za Serikali ziko changamoto zinazokabili makundi haya ya vijana, lakini pia walemavu na wanawake. Mpango wetu ni kuhakikisha kwamba makundi haya nayo yanakuwa na eneo ambalo wanaweza kwenda kupata mikopo hiyo.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niendelee kuwapa faraja Watanzania kwamba Serikali imeendelea kuzungumza na benki kwa maana ya taasisi za fedha kufungua madirisha ya kutoa mikopo ya viwango mbalimbali kulingana na mahitaji ya mteja mwenyewe na huku ndiko ambako pia tunaruhusu hili kundi la watu kutoka miaka 35 na kuendelea ili kuweza kupata mikopo na kwa hiyo, kadiri Serikali itakapokuwa na uwezo itaendelea kufungua milango na kuanzisha mifuko mingine ili kutoa fursa kwa makundi mengi zaidi kupata mikopo kama mitaji kwa ajili ya shughuli zao za ujasiriamali.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister