Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 32 Water and Irrigation Wizara ya Maji 280 2022-05-27

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kujenga mradi wa maji wa vijiji tisa vya Kata za Oldonyosambu na Oldonyowas?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu, Mbunge wa Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza mradi wa maji wa Oldonyosambu kwa ajili ya kuhudumia vijiji tisa vya kata za Oldonyosambu na Oldonyowas. Utekelezaji wa mradi huo unahusisha ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 47.8, ujenzi wa matanki matatu yenye ujazo wa lita 575,000, ujenzi wa vituo vitatu vya kuchotea maji na booster stations mbili. Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022 na kuimarisha upatikanaji wa huduma ya maji katika kata hizo.