Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 33 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 290 2022-05-30

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanzisha Mkoa wa TANESCO katika Wilaya ya Kahama na kujenga Ofisi ya TANESCO Halmashauri?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, TANESCO imekuwa ikifungua Ofisi za Mikoa na Wilaya katika maeneo mbalimbali nchini kwa kuzingatia mahitaji na vigezo muhimu ikiwa ni pamoja na Wilaya, ongezeko la wateja, ukubwa wa mtandao na miundombinu ya umeme katika maeneo husika. Katika Halmashauri ya Mji wa Kahama ipo Ofisi ya TANESCO ya Wilaya ya Kahama inayotoa huduma kwa wananchi wa Mji wa Kahama pamoja na Halmashauri za Msalala na Ushetu.

Mheshimiwa Spika, katika hatua ya kusogeza huduma zaidi kwa wananchi, TANESCO imefungua Ofisi ndogo yaani Sub Offices katika maeneo ya Nyamilangano, Ilogi na Isaka. TANESCO inaendelea kuongeza Ofisi ndogo nyingine katika maeneo ya Segese, Bulungwa, Bulige na Chambo pamoja na kuongeza watumishi, magari na majengo. TANESCO inaendelea na tathmini ya mahitaji na vigezo kwa ajili ya kufungua Ofisi ngazi ya Mkoa katika Mji wa Kahama.