Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 33 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 291 2022-05-30

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA K.n.y. MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatoa Vitambulisho vya NIDA kwa wananchi wa Mkoa wa Kigoma hususan Jimbo la Muhambwe?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Florence George Samizi, Mbunge wa Muhambwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imesajili jumla ya wananchi 975,844 katika Mkoa wa Kigoma wakiwemo wananchi wa Jimbo la Muhambwe na jumla ya vitambulisho 123,962 vimezalishwa kwa ajili ya wananchi wa mkoa huo. Katika Jimbo la Muhambwe ambalo liko katika Wilaya ya Kibondo, wananchi 139,588 walitambuliwa na vitambulisho 5,126 vilitolewa na kugaiwa kwa wananchi. Serikali inatarajia kukamilisha utoaji wa vitambulisho kwa wananchi wote wenye sifa katika mwaka wa fedha 2022/2023. Nashukuru.