Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 34 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 299 2022-05-31

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaboresha miundombinu ya vituo vya polisi vya Ilongero, Ngamu, Ngimu, Msange na Mtinko katika Jimbo la Singida Kaskazini?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimwa Abeid Ramadhan Ighondo, Mbunge wa Singida Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua uchakavu wa vituo vya polisi vya Ilongero, Mtinko na Ngamu. Tathmini iliyofanyika imebaini kuwa kiasi cha fedha shilingi 46,480,000 zinahitajika ili kugharamia ukarabati wa vituo hivyo. Katika maeneo ya Ngimu na Msange hakuna maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya vituo vya polisi. Napenda kutumia fursa hii kuishauri Halmashauri ya Wilaya ya Singida itenge maeneo yenye ukubwa stahiki pamoja na kutoa hatimiliki ili kuwezesha Serikali kupanga na kutelekeza kazi ya ujenzi wa vituo vya polisi kwenye maeneo hayo kwa kushirikiana na wadau. Nashukuru.