Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 35 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 309 2022-06-01

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG'ENDA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukiendeleza Chuo cha Hali ya Hewa kilichopo Kigoma ili kiwe Chuo Kikuu kishiriki cha Dar es Salaam na kiweze kutoa taaluma nyingine?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kilumbe Shabani Ng'enda, Mbunge wa Kigoma Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania imeendelea na jitihada za kukiendeleza Chuo cha Taifa cha Hali ya Hewa kuwa Chuo Kikuu kishiriki cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Tayari andiko kwa maana ya dhana concept note kuhusiana na ushirikiano huo limeandaliwa na Chuo cha Taifa cha Hali ya Hewa (NMTC) na kuwasilishwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ahsante.