Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 35 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 310 2022-06-01

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: -

Je, Serikali imetekeleza kwa kiwango gani Mkakati wa Afrika wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (STISA – 2024) kufuatia maendeleo makubwa ya sayansi, teknolojia na ubunifu duniani?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA, alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nusrat Shaaban Hanje, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilianza kutekeleza Mkakati wa Afrika wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu uitwao STISA 2024 mwaka 2015 kwa kuandaa mpango wa utekelezaji wa mkakati husika. Utekelezaji umejikita katika maeneo yafuatayo; eneo la kwanza ni kuweka mazingira wezeshi ya watafiti na wabunifu kwa ujumla kwa kutenga fedha kila mwaka kwa ajili ya utafiti na ubunifu kupitia Mfuko wa Taifa wa Uendelezaji wa Sayansi na Teknolojia yaani MTUSATE; eneo la pili ni kuimarisha miundombinu ya utafiti na ubunifu kwa kuongeza idadi na kuwajengea uwezo watafiti na wabunifu kupitia miradi mbalimbali ikiwemo Mradi wa Vituo vya Umahiri yaani ACE-II; Mradi wa Kukuza na Kuendeleza Ujuzi (ESPJ); Mradi wa Afrika Mashariki wa Kuboresha Mafunzo ya Ufundi (EASTRIP) na Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mabadiliko ya Uchumi (HEET); na eneo la tatu ni kuimarisha mahusiano kati ya Taasisi za ubunifu /utafiti na sekta za viwanda, nakushukuru sana.