Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 35 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 313 2022-06-01

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kuhakikisha Maporomoko ya Kalambo yanatangazwa ili yawe na mchango wa kiuchumi kwa Taifa?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege Mbunge wa Jimbo la Kalambo kama ifuatavyo:-

Katika kuhakikisha maporomoko ya Kalambo yanatangazwa kikamilifu, hatua zifuatazo zimeanza kuchukuliwa. Hatua ya kwanza ni kutumia vyombo vya habari kuandaa machapisho na majarida kushiriki katika maonyesho matamasha matukio na makongamano ya utalii na biashara yanayofanyika ndani na nje ya nchi. Aidha, jumla ya watalii 2,365 walitembelea maporomoko hayo mwaka 2021 ikilinganishwa na watalii 300 kwa mwaka 2016 na kuweka mabango katika viwanja vya ndege ikiwemo Uwanja wa Ndege wa Songwe na maeneo mengine katika Mkoa wa Rukwa.