Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 35 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 314 2022-06-01

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: -

Je, kuna mango gani wa kudhibiti Tembo wanaoharibu mazao na kujeruhi wananchi Kata za Mindu, Kahulu na Tinginya -Tunduru?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante; kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, Mbunge wa Viti maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Vijiji vingi katika Wilaya ya Tunduru vinapakana na Hifadhi ya Taifa ya Nyerere na ushoroba wa wanyamapori wa Selous Niassa ambao ni mapito ya wanyamapori kati ya Tanzania na Msumbiji.

Mheshimiwa Spika, Wizara imechukua hatua zifuatazo: -

(i) Kuomba kibali cha kuajiri Askari wapya 600 ambao watasambazwa kwenye maeneo hatarishi ili kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu. Sambamba na hilo, Wizara ina mkakati wa kuanzisha vituo vya kikanda vya Askari katika maeneo yenye changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu;

(ii) Kutoa mafunzo kwa askari wa wanyamapori wa vijiji; na

(iii) Kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna bora ya kupunguza athari zinazotokana na wanyamapori wakali na waharibifu.