Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 36 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 316 2022-06-02

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: -

Je, ni lini Kata ya Kwihancha itapata Kituo cha Afya na ni lini huduma za afya zitaimarishwa katika Hospitali ya Nyamwaga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Mwikwabe Waitara, Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022, imetenga Shilingi Milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje (OPD) na Maabara katika kituo cha afya. Fedha hiyo itapelekwa kabla ya tarehe 30 Juni, 2022. Aidha katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga shilingi Milioni 400 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa kituo hicho.

Mheshimiwa Spika, huduma za afya katika Hospitali ya Nyamwaga zinaendelea kuimarika ambapo Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022, imetenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa hospitali hiyo. Ujenzi wa wodi mbili za wanaume na wanawake umekamilika na ujenzi wa majengo ya maabara, wodi ya watoto na jengo la kuhifadhia dawa upo katika hatua za umaliziaji. Aidha, huduma zinaendelea kutolewa ikiwemo huduma za uzazi na upasuaji.