Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 36 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 317 2022-06-02

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ukarabati wa Stendi Kuu ya Mabasi Bweri iliyopo Manispaa ya Musoma?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ghati Zephania Chomete, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Stendi ya Mabasi ya Bweri katika Manispaa ya Musoma ilijengwa mwaka 2007 kwa mapato ya ndani ya halmashauri kwa kutumia Mkandarasi CMG Construction Company Limited aliyeingia Mkataba wa shilingi bilioni 1.36 ambapo Mkandarasi huyo alifanya kazi zenye thamani ya shilingi milioni 921.17.

Mheshimiwa Spika, lengo la Serikali ilikuwa kujenga stendi hiyo kupitia ufadhili wa Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Afrika (BADEA). Hata hivyo kutokana na majadiliano kutozaa matunda, Serikali imeiweka stendi hiyo kwenye Mpango wa TACTIC ambapo shilingi bilioni 1.35 zimetengwa.