Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 36 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 318 2022-06-02

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA K.n.y MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-

Je, Serikali ina kauli gani kuhusu mikopo inayotolewa na Halmashauri kwa kuwa mfumo unawaacha nje vijana wengi kwa kukosa sifa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kanuni ya 6 ya Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo ya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu ya Mwaka 2018 pamoja na marekebisho yake inaelekeza sifa na vigezo vya kuzingatiwa kwenye utoaji mikopo kwa vijana.

Mheshimiwa Spika, vigezo na sifa hizo ni pamoja na kikundi kinachofanya shughuli za ujasiriamali au kinachotarajia kuanza shughuli hizo, Kikundi kiwe kimetambuliwa kama kikundi cha vijana; Wanakikundi wawe Watanzania wenye umri kati ya miaka 18 hadi 35; Kikundi cha vijana kiwe na idadi ya wanakikundi kuanzia watano (5) na kuendelea; Kikundi kiwe na akaunti ya benki iliyofunguliwa kwa jina la kikundi kwa ajili ya matumizi ya kikundi; na Kikundi hakitajumuisha wajumbe wenye ajira rasmi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia sifa hizo, katika mwaka wa fedha 2021/2022, jumla ya Vikundi 1,441 vya Vijana vilikopeshwa mikopo yenye thamani ya shillingi Bilioni 13.5 nchini kote.

Mheshimiwa Spika, kauli ya Serikali ni kwamba, vijana wenye sifa tajwa waendelee kujiunga katika vikundi vya wajasiriamali na kuomba mikopo hiyo ili kuinua uchumi wao. Ahsante.