Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 36 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 320 2022-06-02

Name

Dr. Paulina Daniel Nahato

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza miundombinu ya Vyuo Vikuu nchini kutokana na ongezeko kubwa la wanafunzi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Paulina Daniel Nahato, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mradi wa Higher Education for Economic Transformation (HEET) itajenga Chuo Kikuu kipya cha Kilimo na Teknolojia cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Butiama chenye uwezo wa kudahili wanafunzi 5,620. Vilevile Kampasi mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Mkoa wa Lindi kitakachokuwa na uwezo wa kubeba wanafunzi 360, Kampasi mpya ya Mloganzila ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili wanafunzi 11,000, Kampasi mpya ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo cha Mizengo Pinda Mkoa wa Katavi wanafunzi 2,500, Kampasi mpya ya Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya Kampasi ya Rukwa wanafunzi 3,000. Vilevile, mradi wa HEET utafanya ujenzi wa Kampasi mpya za Vyuo Vikuu katika Mikoa ya pembezoni ikiwemo Mikoa ya Kagera, Tanga, Kigoma, Shinyanga, Mwanza, Simiyu, Ruvuma, Manyara na Singida.

Mheshimiwa Spika, mradi huo kwa ujumla unatarajia kuboresha Taasisi za Elimu ya Juu 19 kwa kujenga Hosteli 34 zenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 9,042, vyumba vya mihadhara 130 vitakavyokuwa na uwezo wa kubeba wanafunzi 27,254, maabara na karakana zitakazokuwa na uwezo wa kubeba wanafunzi 7,850, kumbi za mikutano ya Kisayansi 23, miundombinu ya mashambani pamoja na Vituo Atamizi 10. Nakushukuru sana.