Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 36 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 321 2022-06-02

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa mpaka kati ya Kambi ya Jeshi 845 Itaka na Wananchi wa Vijiji vya Sesenga na Itewe?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa George Ranwell Mwenisongole, Mbunge wa Mbozi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Jeshi Itaka ilikuwa ni mashamba ya walowezi wa kikoloni (settlers), yaliyotwaliwa na Serikali kwa mujibu wa sheria. Mashamba hayo yaligawiwa kwa Jeshi kati ya mwaka 1980 na 1981. Mashamba hayo yalikuwa chini ya umiliki wa Jeshi la Kujenga Taifa Kambi ya Itende. Baada ya mafunzo ya JKT kusitishwa mwaka 1994, wananchi walianza kuvamia na kuendesha shughuli za kibinadamu, hususan kilimo na makazi.

Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Mwenisongole kwa kuendelea kulifuatilia suala hili kwa karibu. Kufuatia ufuatiliaji wake Wizara imeunda Timu ya Wataalam mbayo imepewa jukumu la kuangalia namna bora ya kutatua mgogoro huu. Timu hii ipo uwandani, ikishirikiana na viongozi, lakini pia pamoja na wananchi katika eneo husika. Nimwombe tu Mheshimiwa Mbunge kwa heshima, awe na subira wakati tukisubiri timu hiyo ikamilishe kazi na mapendekezo yawasilishwe na timu hiyo ya wataalam. Ahsante.