Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 36 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 322 2022-06-02

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa bei elekezi ya vifaa vya tiba hasa vya macho, pua na koo?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Mwanaisha Ng’anzi Ulenge, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali imeandaa kanuni za kudhibiti bei za dawa na tayari zimekwishawasilishwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Bei elekezi za vifa tiba zitaandaliwa mara baada ya kukamilika kwa kanuni za bei za dawa elekezi. Ahsante.