Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 36 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 323 2022-06-02

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Daraja la Mto Ruvuma ili kufungua Shughuli za Kibiashara?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. FREDY A. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Selemani Mtenga, Mbunge wa Mtwara Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali za Tanzania na Msumbiji zilijenga Daraja la Umoja (Mtambaswala) ili kufungua shughuli za kibiashara. Kwa sasa Serikali ya Tanzania inategemea kuanza kufanya mazungumzo na Serikali ya Msumbiji, ili kuanza taratibu za ujenzi wa Daraja la Kilambo, Mto Ruvuma.

Mheshimiwa Spika, ahsante.