Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 39 Water and Irrigation Wizara ya Maji 348 2022-06-07

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: -

Mheshimiwa Spika, je, ni lini mradi mkubwa wa maji toka Mto Rufiji utaanza kutekelezwa ili kuwaondolea wananchi wa Kata 23 za Wilaya ya Kilwa tatizo la ukosefu wa maji safi na salama ambalo limekuwa likiwakabili kwa muda mrefu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hali ya upatikanaji huduma ya maji katika Wilaya ya Kilwa ni wastani wa asilimia 64. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi tisa ambayo inatarajiwa kukamilika mwezi wa Julai, 2022 na kuboresha huduma ya maji kufikia asilimia 86.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali itaajiri Mtaalam Mshauri na kufanya usanifu wa mradi wa kimkakati na kwa kutumia chanzo cha maji cha Mto Rufiji ikiwa ni mpango wa muda mrefu wa kuboresha huduma ya maji katika Wilaya ya Kilwa na maeneo mengine ya Mkoa wa Lindi.