Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 40 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 358 2022-06-08

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Manyara?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asia Abdulkarimu Halamga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa jengo la Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Manyara ulianza mwaka 2012 kwa kutumia Mkandarasi aitwaye MS Mavonda’s Co. Ltd kwa gharama ya shilingi 862,167,729. Ujenzi huo ulipofikia asilimia 65 zilijitokeza changamoto katika kutekeleza mkataba hali iliyosababisha kuvunjika kwa mkataba huo mwezi Agosti, 2017.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imepanga kukamilisha utekelezaji wa mradi huo kwa utaratibu wa nguvu kazi kwa maana ya Force Account ambapo taratibu zote zimekamilika na tayari kiasi cha fedha shilingi 353,986,150 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo zimepokelewa kutoka Hazina. Ujenzi wa jengo hilo unatarajia kukamilika mwezi Oktoba, 2022. Nashukuru.