Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 40 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 362 2022-06-08

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha Kilimo katika eneo la Ngongo Mkoani Lindi ambapo tayari hekari 120 zimetengwa kwa ajili hiyo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah, Mbunge Lindi Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kutambua umuhimu wa kuimarisha huduma za ugani iliamua kuanzisha Vyuo Vya Mafunzo vya Kilimo vya Serikali tangu miaka ya 1930 ili kuendeleza sekta hii hapa nchini. Mpaka sasa vimeshaanzishwa Vyuo Vya Mafunzo ya Kilimo 14 ambavyo vinatoa mafunzo ya fani mbalimbali za kilimo ngazi ya Astashahada na Stashahada kikiwepo Chuo cha MATI Mtwara kwa ajili ya Kanda ya Kusini kwa maana ya Lindi na Mtwara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Wizara inaendelea na ukarabati wa Vyuo vya Mafunzo ya Kilimo na kuvipatia vifaa vya kufundishia. Hata hivyo, Serikali kupitia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inatekeleza Mradi wa HEET ambapo katika eneo hilo la Ngongo kitajengwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kampasi ya Lindi kitakachotoa programu za kilimo.