Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 45 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 397 2022-06-16

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza michango kwa Wanafunzi wanaojiunga Kidato cha Kwanza?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Kembaki Michael, Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Waraka wa Elimu Namba 5 wa mwaka 2015 iliamua kutoa Elimu Msingi kuanzia Elimu ya Awali hadi Kidato cha Nne bila malipo. Azma hii ya Serikali ni sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 ambayo ina lengo la kuhakikisha kwamba watoto wote wa Kitanzania wenye rika lengwa la Elimu Msingi wanapata elimu bila kikwazo chochote ikiwemo ada au michango.

Mheshimiwa Spika, michango inayoendelea shuleni kwa sasa ni michango ya lishe ambayo imepata kibali cha Mkuu wa Wilaya baada ya kuidhinishwa na Mkutano Mkuu wa Wazazi. Michango hii ni kwa wanafunzi wote wa Kidato cha Kwanza hadi Kidato cha Nne.