Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 45 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 398 2022-06-16

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tathmini iliyofanyika imebaini kuwa kiasi cha Shilingi 43,000,000 kinahitajika ili kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Dunga kilichoko Wilaya ya Kati, Mkoa Kusini Unguja. Serikali kupitia Jeshi la Polisi inatafuta fedha hizo ili kumalizia ujenzi huo, kama njia ya kuunga mkono juhudi za wananchi na wadau, hususani katika mwaka wa fedha 2023/2024.