Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 45 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 400 2022-06-16

Name

Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaboresha Kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Santiel Erick Kirumba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga kwa sasa ina sehemu maalum yenye uwezo wa kulaza Watoto Njiti 18 kwa wakati mmoja. Hata hivyo, ujenzi unaendelea wa Bilioni 1.2 utakaowezesha hospitali kuwa na vitanda 42. Kwenye bajeti ya mwaka 2022/2023 zimetengwa Shilingi Bilioni Sita kwa ajili ya ujenzi.