Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 3 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 36 2023-11-02

Name

Mwanakhamis Kassim Said

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Primary Question

MHE. MWANAKHAMIS KASSIM SAID aliuliza:-

Je, TFF inashirikianaje na ZFF kupandisha hadhi Ligi ya Zanzibar na kuendeleza vipaji vya wachezaji wa Zanzibar?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwanakhamis Kassim Said, Mbunge wa Jimbo la Magomeni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) chini ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imekuwa ikishirikiana na ZFF katika mipango mbalimbali kwa lengo la kuendeleza Soka la Tanzania. Kwa sasa Bodi ya Ligi ipo katika mchakato wa kuandaa mafunzo ya uendeshaji wa Bodi ya Ligi ya Zanzibar ambayo kimsingi yatalenga namna ya uendeshaji wa Bodi ya Ligi katika masuala ya menejimenti, ligi na masuala ya uwekezaji, udhamini na masoko.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa kuibua vipaji, TFF imekua ikishirikiana na ZFF katika uteuzi wa wachezaji katika timu za Taifa za Vijana, ambapo vijana kutoka Zanzibar wamekuwa wakiitwa katika vikosi vya timu ya Taifa ya vijana na hatimaye kucheza katika timu ya Taifa ya wakubwa (Taifa Stars), ahsante.