Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 3 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 41 2023-11-02

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza:-

Je, upi mpango wa kuboresha Vituo vya Polisi Busanda hususani Kituo cha Katoro na Chigunda?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tumaini Bryceson Magessa, Mbunge wa Busanda kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama maandalizi ya kuboresha vituo vya Katoro na Chigunda, tathmini kwa ajili ya ukarabati na uboreshaji wa mazingira ya vituo hivyo imeshafanyika na kubaini kuwa kiasi cha shilingi 37,265,000 zinahitajika. Fedha hizo tunatarajia kuzitenga kwenye Bajeti ya Serikali ya mwaka 2024/2025 ili kugharamia ukarabati wake.