Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 3 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 43 2023-11-02

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza:-

Je, lini Serikali itapeleka Askari na kulipa fidia kwa Wananchi waliovamiwa na Tembo kwenye makazi na mashamba yao Jimbo la Igalula?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Jimbo la Igalula, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) imeweka askari sita wakiwemo askari wa uhifadhi wawili na askari wa vijiji (VGS) wanne katika kituo cha kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu cha Ndala kilichopo katika Wilaya ya Nzega mkoani Tabora. Aidha, askari hao wamepewa vitendea kazi ikiwemo pikipiki mbili na silaha ambavyo vinawawezesha kudhibiti wanyamapori hao popote wanapoonekana ikiwemo Jimbo la Igalula.

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikilipa kifuta jasho na kifuta machozi kwa wananchi wanaopata madhara kutokana na Wanyama pori ambapo kwa upande wa Wilaya ya Uyui ambayo inajumuisha Jimbo la Igalula Wizara imepokea maombi ya wananchi 17 waliopata madhara ya wanyama pori wakali na waharibifu, maombi hayo kwa sasa yanaendelea kufanyiwa kazi.

Mheshimiwa Spika, kupitia Bunge lako tukufu niendelee kutoa rai kwa wakurugenzi wa Halmashauri wa wilaya hususan zenye changamoto za wanyama pori wakali na waharibifu kuharakisha kuwasilisha maombi yanayotokana na madhara ya Wanyama pori hao Wizarani ndani ya siku saba ili kuiwezesha Serikali kufanya malipo ya kifuta jasho na kifuta machozi kwa wakati.