Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 46 Water and Irrigation Wizara ya Maji 404 2022-06-17

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. SALMA R. KIKWETE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Jimbo la Mchinga kutoka kwenye chanzo cha maji cha Ng’apa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salma Rashid Kikwete, Mbunge wa Jimbo la Mchinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imeendelea kuboresha huduma ya maji katika Manispaa ya Lindi kwa kujenga miradi ya maji inayotumia chanzo cha visima vya Ng’apa. Maji yamefika eneo la Mitwero na kazi inayoendelea ni kuyafikisha maji Mchinga ambapo Kata za Mchinga, Mvuleni, Kilolambwani na Kilangala zenye jumla ya vijiji 18 zitanufaika.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, wananchi katika vijiji nane katika Kata ya Mbanja inayopitiwa na bomba kuu kwenda Mchinga watanufaika. Kwa sasa, Mkandarasi anaendelea na kazi. Kazi zinazoendelea ni ulazaji wa bomba kuu umbali wa kilometa 42, ulazaji wa mabomba ya usambazaji kilometa 12.9 na ujenzi wa matanki manne yenye ujazo wa lita 100,000, mawili yenye ujanzo wa lita 200,000 na moja la lita 680,000. Kazi hiyo inatarajiwa kukamilika katika mwaka wa fedha 2022/2023.