Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 46 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 407 2022-06-17

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Old Shinyanga kupitia Iselamagazi, Solwa hadi Salawe kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christina Christopher Mnzava, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa sehemu ya Solwa - Salawe yenye urefu wa kilometa 15.35. Kwa sehemu iliyobaki kutoka Solwa kwenda Iselamagazi hadi Old Shinyanga yenye urefu wa kilometa 64.66 kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina inaendelea. Baada ya kazi ya usanifu kukamilika na gharama ya ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha ili kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami. Ahsante.