Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 46 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 408 2022-06-17

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KABULA E. SHITOBELA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapunguza tozo zinazotozwa na TPA kwani imekuwa ikitoza tozo kubwa kwenye mizigo kuliko Makampuni binafsi?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE FREDY MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kabula Enock Shitobela, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kuhakikisha Bandari zote za Tanzania zinatoa huduma bora na kwa gharama nafuu ili kuendana na hali halisi ya ushindani katika bandari za ukanda wa Afrika Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika. Katika kufikia azma hiyo, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ipo katika hatua za mwisho za kufanya mapitio ya gharama za huduma za bandari. Hivi sasa, uchambuzi wa maoni yaliyowasilishwa na wadau mbalimbali yanafanyiwa kazi na zoezi hili linatarajiwa kukamilika Julai, 2022.