Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 4 2023-10-31

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa majengo ya zahanati Kijiji cha Masagalu Mission, Kilindi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua, Mbunge wa Jimbo la Kilindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2018/2019 Serikali ilipeleka shilingi milioni 100 katika Halmashauri ya Kilindi kwa ajili ya kukamilisha boma la Zahanati ya Masagalu. Kwa kuwa boma hilo lilijengwa kwa ramani ya zamani ambayo ni kubwa zaidi, ujenzi haukuweza kukamilika.

Mheshimiwa Spika, Zahanati ya Masagalu imeanza kutoa huduma kwenye baadhi ya vyumba ambavyo vimekamilika. Aidha, Serikali kupitia Mapato ya ndani ya Halmashauri ya Kilindi itatenga shilingi millioni 100 katika Mwaka wa Fedha 2024/2025 ili kukamilisha ujenzi, ahsante.