Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 127 2023-11-09

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka lami walau kilometa 10 za barabara za ndani za Mji wa Katesh ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NGEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Samweli Hhayuma, Mbunge wa Jimbo la Hanang’ kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TARURA imeanza utekelezaji wa ahadi hiyo ambapo kwa mwaka wa fedha 2021/2022, jumla ya shilingi milioni 470.61 zimetumika katika ujenzi wa barabara kilometa 1.12 kwa kiwango cha lami. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, jumla ya kilometa 0.7 zimejengwa kwa kiwango cha lami na shilingi milioni 499.91 zimetumika. Kwa upande wa mwaka wa fedha 2023/2024, jumla ya ya shilingi milioni 941.96 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa kilometa 1.2 na utekelezaji umefikia asilimia 30.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti kulingana na upatikanaji wa fedha ili kukamilisha ahadi hiyo ya kukamilisha ujenzi wa kilomita 10 za barabara kwa kiwango cha lami.