Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 47 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 416 2022-06-20

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itasaidia kukarabati mifereji ya Marwa, Kwasita, Magereza, Gunge na Kirua katika Bonde la Mto Pangani?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Bonde la Mto Pangani katika uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara. Bonde hili ni pamoja na skimu nyingine pia linajumuisha skimu za Kirya, Marwa, Kwasita, Magereza, Gunge, Kirua na Ruvuna kwa upande wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali inaendelea na ujenzi wa skimu ya Kirya ambayo inatarajiwa kukamilika mwaka 2022/2023. Katika mwaka wa Fedha 2023/2024, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Skimu za Marwa, Kwasita, Magereza, Gunge na Kirua ili kujua gharama halisi za ukarabati na ujenzi wa skimu hizo.