Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 42 Education, Science,Technology and Vocational Training, Ofisi ya Rais TAMISEMI. 356 2016-06-14

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO (K.n.y. MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA) aliuliza:-
Shule ya Sekondari ya Ndembela Wilayani Rungwe awali ilijengwa kwa nguvu za wananchi na baadaye Kanisa la Waadventista Wasabato liliingia kama wabia na kuiendeleza na hatimaye kuiendesha shule hiyo ikiwa na majengo yaliyokamilika. Baada ya wananchi kuihitaji shule yao, Kanisa limekubali kuirejesha kwa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa fidia ya Sh.947,862,000/= Halmashauri imeomba Wizara ya Elimu isaidie kulipa fidia hiyo:-
Je, ni lini Serikali itasaidia kurejesha shule hiyo mikononi mwa wananchi kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, thamani halisi ya majengo ya Shule ya Sekondari Ndembela ni shilingi milioni 762 baada ya tathmini. Mwaka 2013, Kanisa la Waadventista Wasabato na Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe walikubaliana mbele ya Mahakama kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe ilipe fidia ya shilingi milioni 762 ikiwa ni thamani halisi ya maendelezo yaliyofanyika ili shule iweze kurejeshwa kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017, Halmashauri imeidhinishiwa shilingi milioni 190 kwa ajili ya kulipa sehemu ya deni hilo. Aidha, Halmashauri imewasilisha maombi maalum ya shilingi milioni 947.8 katika Mamlaka ya Elimu Tanzania yaani TEA kwa ajili ya kulipa fidia na ukarabati wa miundombinu ya shule.