Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 109 2024-02-07

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza:-

Je, lini Serikali itamalizia ujenzi wa zahanati ya Uwanja wa Ndege katika Kata ya Mafisa Mkoani Morogoro?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Norah Waziri Mzeru, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kusogeza huduma za afya kwa wananchi wa Uwanja wa Ndege, mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali ilipeleka shilingi milioni 70 kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati ya Uwanja wa Ndege iliyopo katika Kata ya Kiwanja cha Ndege Manispaa ya Morogoro. Ujenzi umekamilika na huduma zimeanza kutolewa mwezi Mei, mwaka 2022. Zahanati hii kwa wastani huhudumia wagonjwa wapatao 750 kwa mwezi na wagonjwa 9,000 kwa mwaka, ahsante.