Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Planning and Investment Ofisi ya Rais: Mipango na Uwekezaji 111 2024-02-07

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuvutia wawekezaji kujenga viwanda vya maziwa Mkoa wa Arusha?

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zaytun Seif Swai, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, fursa za ujenzi wa viwanda vya maziwa katika Mkoa wa Arusha hutangazwa kupitia makongamano ya uwekezaji yanayoratibiwa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC). Vilevile, Kituo hiki huandaa safari na mikutano ya uwekezaji nje ya nchi ambapo hutangaza fursa za uwekezaji zilizopo nchini ikiwa ni pamoja na fursa za uwekezaji wa viwanda vya kusindika maziwa katika Mkoa wa Arusha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia kampeni ya kitaifa ya kuhamasisha uwekezaji nchini, Watanzania wanahimizwa kuendelea kuwekeza nchini kwa kutumia malighafi zilizopo katika maeneo yetu husika, nakushukuru.