Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 116 2024-02-07

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza: -

Je, lini miundombinu ya mipaka ya nchi yetu itaboreshwa ili kukuza diplomasia ya uchumi na nchi zenye fursa za kibiashara kama DR – Congo?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Felista Deogratius Njau, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia TANROADS inaendelea na ujenzi na ukarabati wa barabara zinazounganisha nchi yetu na nchi zote jirani ikiwemo nchi ya DRC kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Serikali imekamilisha ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Sumbawanga – Matai hadi Bandari ya Kasanga yenye urefu wa kilometa 107 Mkoani Rukwa na tayari Serikali imesaini mkataba wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Kigwira – Karema yenye urefu wa kilometa 112 kwenda bandari ya Karema mkoani Katavi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali inatekeleza mpango wa kuboresha barabara ya kuanzia Igawa – Mbeya - Tunduru kuwa njia nne, mkandarasi yupo site. Serikali inaendelea kuboresha viwanja vya ndege vya Songwe, Sumbawanga na Kigoma ambavyo vipo mpakani na DRC. Kwa hiyo, yote hii ni katika kuiunganisha nchi yetu pamoja na DRC, ahsante sana.