Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 4 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 48 2023-11-03

Name

Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza:-

Je, Serikali ipo tayari kuleta marekebisho ya Sheria baada ya Serikali kukubaliana kuondoa baadhi ya changamoto za Muungano?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zahor Mohammed Haji, Mbunge na mtumishi wa Wananchi wa Jimbo la Mwera kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Changamoto zote za Muungano zimekuwa zikitatuliwa na kupatiwa ufumbuzi kwa njia ya Majadiliano na Maridhiano utaratibu ambao umekuwa na mafanikio makubwa. Aidha, katika utatuzi wa Changamoto hizo umeandaliwa utaratibu wa vikao vya Kamati ya Pamoja ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa ajili ya kushughulikia Masuala hayo ya Muungano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu huu umetumika kwa mafanikio makubwa na kuhakikisha changamoto nyingi za Muungano zinatatuliwa. Hata hivyo, ushauri wa Mheshimiwa Mbunge ni mzuri na Serikali inaangalia uwezekano wa kufanya vikao vya pamoja baina ya SJMT na SMZ ili changamoto zilizotatuliwa kupewa na nguvu ya kisheria, nakushukuru.