Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 174 2024-02-13

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kujenga barabara ziendazo maeneo ya mazao ya kimkakati kama chai, kupitia mradi wa Agri-Connect - Lupembe?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Edwin Enosy Swalle, Mbunge wa Jimbo la Lupembe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imeainisha barabara zinazopita kwenye maeneo ya mazao ya kimkakati, ikiwemo zao la chai katika Jimbo la Lupembe, ambazo zina urefu wa jumla ya Kilometa 182.5. Kwa Mwaka wa fedha 2023/2024, usanifu wa Barabara ya Ukalawa – Kanikelele – Lupembe yenye urefu wa Kilometa 18.5, upo hatua za mwisho kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea na mpango wake wa kutenga bajeti ili kuboresha barabara kwenye maeneo ya mazao ya kimkakati ikiwemo Jimbo la Lupembe. (Makofi)